Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

© UNICEF/Saleh Hayyan

Mkimbizi wa ndani nchini Yemen aliyepata ajali akiwa kazini asema hajakata tamaa

Nchini Yemen maisha ya ufukara ni dhahiri miongoni mwa wakimbizi wa ndani ambapo hata kwa wale ambao walibahatika kupata vibarua, ajali kazini imeleta madhila na machungu zaidi na kuzidi kutia mashaka mustakabli wa watoto nchini humo kama anavyosimulia Anold Kayanda
(Taarifa ya Anold Kayanda)

Upepo unavuma katika kambi ya wakimbizi ya Al Shaheed jimboni Al Mukha nchini Yemen. Abdullah Jaber anarejea kwenye kibanda chake cha mabati kisicho hata na paa, akiwa na kile kitakachokuwa mlo wa siku kwa familia yake ya mke na watoto wawili.

Sauti
2'7"
World Bank/Tom Perry

Kupiga makasia na kula samaki mwarobaini wa unene uliopiliza nchini Tonga

Nchini Tonga, moja ya mataifa ya visiwa vidogo lililoko katika bahari ya Pasifiki, vijana wanafundishwa stadi ya utengenezaji mitumbwi kama njia mojawapo ya kujipatia kipato, kulinda mazingira na kupunguza unene uliopitiliza au utipwatipwa. Kwa vipi? 

(Taarifa ya Leah Mushi)

Katika karakana ya utengenezaji wa mitumbwi nchini Tonga, taifa lenye visiwa vidogo 170 na ambako chakula si mazao yalimwayo nchini humo bali kwa kiasi kikubwa vilivyosindikwa na hivyo kusababisha kuwa moja ya nchi yenye watu wengi tipwatipwa duniani.

Sauti
2'27"
UNICEF/Sigfried Modola

Programu ya UNICEF Turkana yawasaidia watoto wa kike kurejea shuleni

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto duniani UNICEF kwa kushirikiana na serikali ya Kenya wanaendesha programu maalum ya “Elimisha mtoto” inayowachagiza wazazi na watoto wa kike waliocha shule wakati wa janga la corona au COVID-19 na kwa sababu ya mimba za utotoni, na sababu nyingine kurejea shuleni. 
 
(TAARIFA YA FLORA NDUCHA) 
Nattss…. 

Sauti
2'46"
UNICEF/Josue Mulala

Lokua Kanza aingia darasani Kinshasa na ujumbe mzito wa elimu kwa wanafunzi

Lokua Kanza, mwanamuziki nguli ndani  na nje ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye pia ni balozi wa kitaifa wa elimu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo, ametumia ziara yake katika shule ya msingi aliyosoma utotoni ili kuchagiza wanafunzi wa kike na wa kiume kupatia kipaumbele suala la elimu. 

Sauti
2'22"
© WFP/Arete/Fredrik Lerneryd

DRC yakamilisha vigezo vya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki

Wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa nchi duniani kuimarisha ushirikiano wa kimataifa iwe kikanda au kidunia unazidi kuitikiwa ambapo Jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC inachukua hatua kupanua wigo wa uanachama wake kutoka 6 hadi 7 kwa kufanya kikao cha kujadili ombi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kujiunga na chombo hicho.

Sauti
2'9"
UN

WHO na wadau wataka hatua zaidi kukabili homa ya uti wa mgongo

WHO na wadau wataka hatua zaidi kukabili homa ya uti wa mgongo
Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO na wadau wake wamezindua mkakati wa kwanza wa aina yake wa kutokomeza ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo, ugonjwa ambao unaua mamia ya maelfu ya watu kila mwaka. Mkakati huo, kwa mujibu wa WHO utaokoa maisha ya zaidi ya watu 200,000 kila mwaka.

Sauti
2'17"
MONUSCO/Michael Ali

Balozi wa Tanzania nchini DRC awatia moyo wananchi wanaolindwa na kikosi cha TANZBATT-8

Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Luteni Jenerali Mstaafu Paul Meela amewasihi wananchi kuwa na imani kuwa matatizo yataisha kwani vikosi vya Umoja wa Mataifa vya kulinda amani nchini humo MONUSCO na Umoja wa Mataifa wenyewe wanafanya juu chini kunakuwa kuhakikisha na amani.  

Ameyasema hayo wakati wa tukio maalum la Afrika Kusini kuikabidhi Tanzania ukamanda wa kikosi cha kujibu mashambulizi FIB kilicho ndani ya MONUSCO, jukumu ambalo makamanda hao hukabidhiana kila mwaka.

Sauti
2'58"