Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UN Women

Tuna uwezo wa kutokomeza ndoa za utotoni Malawi- Chifu Kachindamoto

Nchini Malawi karibu nusu ya wasicha wote huolewa kabla ya kutimiza umri wa miaka 18 na hivyo hukosa elimu, hukabiliwa na ndoa za utotoni na pia athari nyingine kubwa za kiafya ikiwemo fistula na hata kupoteza maisha kutokana na kujifungua wakiwa na umri mdogo.  Sasa wanaharakati wamelivalia njuga sula hilo ambalo mzizi wake ni mila na desturi. ANOLD KAYANDA anatupasha zaidi

Sauti
2'12"
ITU/D. Procofieff

Akili Bandia yaanza kuleta mabadiliko chanya kwenye sekta ya afya nchini Tanzania

Mkutano wa tatu wa kimataifa kuhusu akili bandia, au AI ukiendelea huko Geneva, Uswisi, nchini Tanzania inaelezwa kuwa tayari akili bandia imeanza kutumika kuboresha huduma za afya hasa katika maeneo yenye uhaba wa daktari.

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa Castory Munishi, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba, Muhimbili, MUHAS nchini Tanzania, chuo ambacho hivi karibuni kiliendesha mdahalo kuhusu akili bandia na nafasi yake katika kuimarisha huduma za afya.

Audio Duration
2'4"
UNFCCC/James Dowson

Tuzo ya Charlemagne kwangu msingi wake ni wanawake na wanaume wa UN- Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amepokea tuzo ya Charlemangne huko mjini Aachen nchini Ujerumani na kusema kuwa ni heshima kubwa sana kwake na kwa chombo anachoongoza. Grace Kaneiya na ripoti kamili.

Tuzo hiyo ambayo hutolewa kila mwaka tangu mwaka 1950, ni kwa ajili ya watu ambao wanaonekana wako mstari wa mbele kufanikisha muungano wa bara la Ulaya ambapo Guterres katika hotuba yake ya kupokea tuzo hiyo amesema, “ninatambua kuwa mnanituza kupitia mimi kutokana na ahadi, huduma na kujitolea kunakofanywa na wanawake na wanaume walioko Umoja wa Mataifa.”

Sauti
1'59"
UNnewskiswahili/Patrick Newman

Mtandao wa Twitter umeiwezesha IBUA Afrika kuwasaidia vijana: Mumbi

Katika zama hizi ambazo kunashuhudiwa mabadiliko katika teknolojia na hata matumizi ya mitandao ya kijamii na huku kuiwa na mwamko wa vijana kujitokeza kuwa wabunifu na kudhihirisha ajira si lazima kuajiriwa  , vijana wameanzisha miradi mbali mbali wakitumia mitandao ya kijamii na teknolojia za kisasa na ambazo zimewasaidia kubadili maisha yao na kuletea kipato. 

Sauti
4'4"
WHO/Marcelo Moreno

WHO yatoa wito wa usikubali tumbaku ichukue pumzi yako.

Kuelekea maadhimisho ya siku ya kimataifa duniani ya kutovuta tumbaku keshokutwa Ijumaa, shirika la afya ulimwenguni, WHO  linaangazia madhara ya matumizi ya tumbaku kwa mapafu ya binadamu ikielezwa kuwa zaidi ya asilimia 40 ya vifo vihusianavyo na utumiaji wa tumbaku vilihusiana na magonjwa kama saratani, magonjwa sugu ya njia ya hewa na Kifua Kikuu.

Sauti
2'30"