Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kamanda wa TANZBATT-10, Luteni Kanali John Peter Kalabaka akimkabidhi bendera ya Tanzania Luteni Kanali  Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kukabidhiana majukumu ya ulinzi wa amani huko Beni Mavivi jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokra…
TANZBATT-10

Wananchi DRC eleweni na ikubalini dhamira ya UN ya kulinda raia - TANZBATT-11

Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10)  kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.

Sauti
3'28"
Pamela Achieng, Hakimu katika mahakama ya Ngong iliyo katika Kaunti ya Kajiado nchini Kenya.
UN News

Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao jamii ziendelee kunufaika - Hakimu Pamela Achieng

Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani tunavinjari hadi nchini Kenya kumsikia Hakimu Pamela Achieng ambaye azma yake ya kujikita kwenye masula ya kusimamia haki ilichochewa na swali alilojiuliza yeye mwenye ya kwamba  “kama mwanaume anaweza kufanya kazi zinazotambulika hasa za kutetea haki za raia katika mahakama kwanini mwanamke asiweze?”

 

 

Sauti
6'16"
Mamilioni ya watu kote ulimwenguni wanapoanza kuadhimisha mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kwa huzuni huko Gaza na katika eneo lote, wengi wataadhimisha mwezi huu wakikabiliwa na migogoro, kufukuzwa na hofu.
© UNRWA

Ni wakati wa Ramadhan tusitishe uhasama Gaza na Sudan: Guterres

Leo ni mwanzo wa mwezi mktukufu wa Ramadhan ambapo Waislamu kote duniani hudumisha na kuchagiza tunu za amani, maridhiano na mshikamano lakini uhasama unaendelea hususani sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Gaza ambako mauaji , na mashambulizi hayajakoma amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani hii leo. 

Sauti
2'53"
Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama nchini Haiti..
© UNICEF/Ndiaga Seck

Haiti: Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama

Kutoroka gerezani kwa zaidi ya wafungwa 4,500 nchini Haiti mwishoni mwa wiki iliyopita wakiwemo viongozi mashuhuri wa magenge ya uhalifu kukitajwa kuwa tishio la usalama wa taifa, huku huduma muhimu kama afya, elimu zikiendelea kuzorota kila uchao, Umoja wa Mataifa unataka hatua za haraka za jamii ya kimataifa kuzuia taifa hilo kuzidi kutumbukia kwenye ghasia.