Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wahajiri wa Burundi kufadhiliwa makazi na UNHCR

Katika miaka mitano iliopita Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limefadhilia makazi wahamiaji 58,000 waliorejea Burundi kutoka matifa jirani na nchi za kigeni, msaada ambao uliowawezesha kujenga nyumba mpya na kupata matumaini ya maisha bora kwa siku zijazo.

Hapa na pale

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) limeupokea mwaka 2008 kwa hamu kuu ilivyokuwa Baraza Kuu lilipitisha azimio la kuufaya kuwa ni Mwaka wa Kuimarisha Usafi wa Kimataifa, baada ya mashirika ya UM kuthibitisha kwamba watu bilioni 2.6, sawa na asilimia 40 ya idadi ya watu duniani, ikijumuisha watotomilioni 980, hunyimwa mazingira safi, hali ambayo huathiri sana afya na kuzusha maelfu ya vifo vinavyotokana na maradhi ya kuambukiza ambayo yanazuilika.