Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akizungumza na waandishi wa habari jijini Nairobi, Kenya.
UNEP/Duncan Moore

Afrika inaweza kuwa jabalí la nishati jadidifu- Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyeko Nairobi Kenya kushiriki mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mashirika yasiyo ya kiserikali, UNCSC amezungumza na waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine amesema wakati huu ambapo bara la Afrika linakabiliwa na madhara ya mabadiliko ya tabianchi, bara hilo linaweza kuwa jabalí wa uzalishaji nishati jadidifu duniani iwapo litawezeshwa.

Sauti
9'43"
Zahra K Salehe Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji, ICCAO Tanzania akizungumza na wanafunzi.
UN News

ICCAO Tanzania: Shirika la vijana linalosaidia kufanikisha SDGs nchini Tanzania

Mnamo tarehe Mosi Januari mwaka 2016, Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDGs) yalianza kufanyiwa kazi rasmi. Tangu wakati huo watu ulimwenguni kote kwa ngazi tofautifauti wamekuwa wakihaha kuhakikisha kufikia mwaka 2030 malengo hayo yanafikiwa. Na kila mara Makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani yamekuwa uwanja wa wazi kwa wadau kutoka kila pembe ya dunia kuja katika mikutano mbalimbali na kubadilishana uzoefu. 

Sauti
5'17"
Eva Ghamaharo, mkazi wa Kaunti ya  Mto Tana, mnufaika wa mradi wa dharura wa mgao wa fedha kwa manusura wa mafuriko unaotekelezwa na UNICEF Kenya.
UNICEF/James Ekwam

Mafuriko Kenya: Mgao wa fedha waleta matumaini kwa wakazi wa Kaunti ya Mto Tana- UNICEF

Wingu kubwa la mvua likiwa limetanda kwenye mji wa Garsen, ulioko kaunti ya Mto Tana nchini Kenya, Eva Ghamaharo, mama wa watoto watatu anarejea nyumbani akitembea na watoto wake wawili mapacha wenye umri wa miaka mitatu baada ya kununua matumizi ya nyumbani kutoka kioski cha jirani. Watoto hawa wawili mapacha wa kike ni Grace na Jane na wanaonekana na furaha kwani angalau leo mama yao ameweza kuwanunulia kila mmoja pakiti ya maziwa na wanakunywa kwa furaha.

Sauti
2'6"
Baadhi yao wamepumzika baada ya siku yenye shughuli nyingi kwenye Mkutano wa Viongozi wa Dunia.
UN News/Laura Quinones

Wanahabari wana jukumu muhimu la kuelimisha juu ya mabadiliko ya tabianchi: UN

Leo ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani mwaka huu ikibeba maudhui “Vyombo vya Habari kwa ajili ya Sayari: Uandishi wa habari katika kukabiliana na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi”  kwani Umoja wa Mataifa unasema mchango wa wanahabari na vyombo vya habari ni kiini katika kuhabarisha na kuelimisha umma kuhusu changamoto hiyo ya tabianchi. 

Sauti
2'23"