Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Sarah Opendi

Bidhaa za tumbaku lazima zidhibitiwe

Bidhaa za tumbaku zinasababisha madhara mengi sana hususani kiafya. Shirika la afya duniani WHO sasa linataka kila nchi mwanachaka kuchukua hatua madhubuti kudhibiti hali hiyo kwa kuweka sheria na kuzitekeleza.

Sauti
2'28"
Jane John (TBC-Tanzania)

Radio haifi ng'o- Jane John

Ujumbe wa siku ya radio duniani mwaka huu wa 2018 ni Radio na Michezo! Umoja wa Mataifa unataka chombo hicho adhimu kitumike kusaidia watu kuchanua na kuonyesha uwezo wao wote. Miongoni mwa watu ambao radio imeweza kuibua stadi zao ni Jane John, mtangazaji wa kike wa habari za michezo katika shirika la utangazaji nchini Tanzania, TBC. Assumpta Massoi alizungumza na Jane kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam, Tanzania na kuanza kwa kumuuliza manufaa ya radio!

Audio Duration
5'10"
UNICEF/Catherine Ntabadde

Mangariba wadondosha nyembe zao Tanzania, wanaume nao wafungua masikio

Nchini Tanzania harakati za shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA zimesaidia kuepusha wanawake na watoto wa kike siyo tu dhidi ya mila hatarishi ya ukeketaji au FGM, bali pia zimesaidia kubadili mtazamo wa wanaume kuhusu kuoa wanawake ambao hawajakeketwa. Ali Haji Hamad, afisa wa jinsia kwenye ofisi hiyo amezungumza na Assumpta Massoi kwa idhaa hii.

Sauti
6'15"

Nidhamu ni sababu kuu ya mafanikio- Kiba

Vijana! Umoja wa Mataifa unasema kuwa kundi hili ndilo linalopaswa kuwa mstari wa mbele kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Hii ni kwa kuzingatia siyo tu wingi wao hivi sasa bali pia uwezo wao wa kubuni na kugundua teknolojia bora na fanisi za kufanikisha malengo hayo.

Sauti
4'11"