Nilinusurika unyanyasaji ili niwasaidie watoto waliotelekezwa wa Eswatini:Siphiwe
Siphiwe Nxumalo, mfanyakazi wa kujitolea wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP huko Eswatini, alirejea nchini mwake baada ya kumaliza masomo yake katika nchi jirani ya Afrika Kusini ili kusaidia yatima na watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wanaokabiliwa na umaskini na kutelekezwa.