Siku 100 baada ya tetemeko Uturuki na Syria, mamilioni ya watoto na familia zao bado wanahaha: UNICEF
Siku mia moja baada ya kutokea kwa matetemeko mabaya zaidi ya ardhi katika historia ya hivi karibuni nchini Uturuki na Syria, mamilioni ya watoto na familia zao wanahaha kujenga upya maisha yao, huku watoto milioni 2.5 huko Uturuki na milioni 3.7 nchini Syria wakihitaji msaada wa kibinadamu unaoendelea limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.