Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News/Patrick Newman

COVAW yabadili maisha ya wasichana wa kaunti ya Kwale

Utalii wasifika sana kwa kuinua kipato cha nchi ya Kenya iliyoko Afrika Mashariki. Hata hivyo baadhi ya watalii wawe wa ndani au wa nje wanatumia fursa hiyo kutekeleza mambo yanayokiuka haki za binadamu hususan kufanya biashara ya ngono. Kutokana na umaskini baadhi ya wasichana kwenye kaunti ya Kwale huko Mombasa, wametumbukia katika mtego wa biashara ya ngono au hata biashara ya binadamu na kujikuta na madhila makubwa zaidi. Shirika moja la kiraia linalopinga ukatili na ghasia dhidi ya wanawake nchini Kenya, COVAW limechukua hatua. Je ni hatua gani?

Sauti
3'53"
Picha ya UN

Kampeni ya kupanda miti Bujumbura

kampeini ya kupanda miti na maua katika barabara za mjini Bujumbura Burundi inafanywa na wakwerekertwa wa mazingira pamoja na kuwahusisha vijana. Pia na Meya wa mji huo ameshiriki katika kampeini ya wiki mbili.

Sauti
3'5"
Picha/UNAIDS

Wakimbizi na ndoto ya kuwa 'Suarez' siku za usoni

Umoja wa Mataifa unakazia michezo kwa maendeleo iwe kwa vijana au wazee, wanawake au wanaume, wasichana au wavulana. Michezo ni mojawapo ya mambo yanayosaidia kumwezesha binadamu kustawi iwe ni kwa kupata ajira kupitia michezo au kuimarisha viungo vyake na wakati mwingine ni burudani. Ni kwa miongoni mwa misingi hiyo, wasichana wakimbizi kutoka Burundi walioko ukimbizini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wameamua kucheza soka na ndoto yao ni kwamba iko siku watacheza viwanja vya kimataifa kama ilivyo akina Suarez!

Sauti
3'6"

Sheria itasaidia kudhibiti matumizi mabaya ya viuavijasumu: Dr Mbindyo

Shirika la afya ulimwenguni WHO linasema matumizi mabaya na ya kupindukia ya viuavijasumu au antibiotic yana athari kubwa sio tu kwa afya ya binadamu na wanyama bali pia katika uchumi. Sasa shirika hilo kwa kushirikiana na shirika la afya ya mifugo OIE wanazichagiza nchi kuchukua hatua ili kuepuka athari hizo kwa kudhibiti matumizi ya dawa za viuavijasumu kwa binadamu na wanyama. Dr Regina Mbindyo ni afisa wa madawa wa WHO nchini Kenya amezungumza na Flora Nducha wa idhaa hii kuhusu athari na jitihada zinazofanyika Kenya kudhibiti matumizi ya dawa hizo.

Audio Duration
3'49"

Teknolojia ya mtandao yatoa ajira kwa vijana Afrika

Ukuaji wa teknolojia ya matandao  leo hii unatoa fursa kubwa ya ajira kwa vijana endapo wataamua kujituma na kuzitumia fursa hiyo vilivyo.

Mfano mzuri ni nchini Ghana ambako vijana wanatumia teknolojia ya mtandao kwa kutengeneza mavazi ya asili maarufu kama  Kente na kuyauza kupitia mtandao baada ya kupata mafunzo ya kibiashara kutoka kwenye taasisi ya maendeleo nchini humo inayotoa mafunzo ya kibiashara. Kwa undani wa makala hiyo unagana na mwandishi wetu Siraji Kalyango.

Sauti
3'24"
YWCA Tanzania

Wanaharakati wakemea wanawake kuvuliwa nguo hadharani Uganda

Ukatili wa kijinsia ni jambo linaloleta hofu kubwa kwa jamii hususan wanawake na watoto wa kike. Ukatili huo ni wa aina mbalimbali ikiwemo wa kingono, kipigo na hata manyanyaso. Mathalani vitendo vya wanawake au wasichana kunyanyaswa kutokana na mavazi yao ni jambo ambalo limekuwa likiripotiwa mara kwa mara maeneo mbalimbali duniani na hivi karibuni matukio kama hayo yaliripotiwa Uganda lakini sauti zilipazwa. Nini kilifanyika? John Kibego ndiye shuhuda wetu.

Audio Duration
3'31"