Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Bima ya afya ni muarobaini wa afya kwa wote- Dkt. Maro

Upatikanaji wa bima ya afya kwa kila mtu ni suala mtambuka  ambalo Umoja wa Mataifa na mashirika yake , wameendelea kulipigua chepuo ili ifikapo mwaka 2030 kila mtu bila kujali rika, uwezo au rangi yake ana uwezo wa  kununua bima ya afya. Utekelezaji wa hoja hiyo unaenda sambamba na mpango wa kimataifa wa kuhakikisha kila mtu anapata huduma ya afya popote pale alipo, UHC au Universal Health Coverage.

Sauti
4'1"

Kazi ni kazi ilimradi inafanywa kwa ustadi

Katika ajenda ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030 , lengo namba 5 la usawa kijinsia, suala ambalo linahimiza jamii kote duniani kuwajumuisha wanawake katika kazi yoyote bila kubagua jinsia, rangi, au rika ya mtu.

Mwandishi wetu anatuletea mfano mzuri nchini kenya  ambako wasichana wameanza kujikita katika kazi ambazo zimezoweleka kufanywa na wanaume. Msichana Tsarah Mumbi kwa sasa ni kivutio kikubwa kwa kila mtu kwa chaguo la kazi analofanya. Unagana na mwandishi wetu kwa undani wa makala hii.

 

Audio Duration
3'44"
UN News/Assumpta Massoi

Ukombozi wa mwanamke kijijini utategemea ushirikiswahi wake:FAO

Ili kuweza kumkomboa mwanamke wa kijijini, ni lazima ashirikishwe katika mchakato mzima, kuanzia utungaji wa sera hadi umilikaji wa ardhi.

Wito huo umetolewa na Bi Susan Kaaria afisa wa masuala ya jinsia katika idara ya sera ya shirika la chakula na kilimo FAO.

Katika makala hii anajadili na Flora Nducha, kama FAO wanafanya nini kufanikisha azma hiyo Ungana nao.

Sauti
3'9"
UN Photo/Sophia Paris

Taka zaepusha matumizi ya dizeli Uganda

Matumizi ya nishati mbadala na salama ni jambo ambalo linapigiwa chepuo na Umoja wa Mataifa ambapo lengo namba 7 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linasisitiza nishati rahisi na salama. Hatua hii inazingatia kwamba idadi ya watu wanaohitaji nishati ya umeme inaongezeka kila siku na hivyo kutoa changamoto ya kusaka vyanzo mbadala vya nishati kwani umeme pekee uliozoeleka ni wa vyanzo vya maji, na ukame unatishia uwepo wa mabwawa ya maji. Ni kwa kuzingatia hilo huko Uganda, wanatumia mabaki ya taka au biomasi ili kuzalisha nishati. Je nini kinafanyika?

Sauti
3'16"
Picha: Luca Renda / UNDP

Utu wetu hudhiirika tunapowasaidia wenye shida

Majanga yanapotokea hua hayapigi hodi, na tunapoamua kuwasaidia waathirka ni jambo jema kwani huo ndio utu wetu. Umoja wa Mataifa na mashirika wadau wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa usaidizi wakati wa migogoro ya kivita, majanga na matatizo  mbambali yanapotokea duniani kote.

leo katika ukumbi wa mikutano wa Umoja wa Mataifa, wafadhili , wahisani  na wageni waalikwa wamekusanyika kutoa usaidizi kwa wahanga wa kimbunga Maria katika visiwa vya karibea mwaka jana . 

Sauti
4'14"
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Ukimkomboa mwanamke, umeikomboa jamii

Nchini Uganda serikali imeamua imechukua hatua ya kuwawezesha wanawake vijijini ili wajiinue kiuchumi lakini pia waache kuwa tegemezi, kwa kuwapa mikopo midogo midogo ambayo inawapa fursa ya kufanyia shughuli za kimaendeleo. Lengo kubwa ni kuhakikisha mwanamke wa kijijini asalii nyuma na kuzama katika lindi la umasikini.

Mwandishi wetu John kibego amewatembelea baadhi ya wanawake hao katika wilaya ya hoima kushuhudia shughili wanazofanya.  Ambatana nao katika Makala hii

Audio Duration
3'13"
Picha ya UNAMA/Fardin Waezi

Wananchi wana wajibu mkubwa wa kuepusha majanga: UN

Ajenda ya malengo ya maendeleo enedelevu SDGs ya mwaka 2030 inahimiza serikali, asasi zakiraia na mashirika ya kibinadamu kuweza kupigia chepuo  suala la ulinzi wa mazingira ili kuepuka majanga kama nvua za kupindukia, vimbunga, mafuriko na kadhalika. Mwandishi wetu kutoka maziwa makuu Ramadhan Kibuga leo ametembelea eneo la Gatunguru nje kidogo ya jiji la Bujumbura Burundi, na kushuhudia athari za tatizo la mvua kubwa za kila wakati na kusababisha maporomoko ya ardhi.

Audio Duration
4'1"

Vijana nchini Zambia ni mfano wa kuigwa katika kilimo

Ufugaji samaki ni biashara inayo wakwamua vijana wengi nchini Zambia na tatizo la ajira. Shirika la kazi duniani ILO na lile chakula na kilimo FAO kwa pamoja na serikali ya Zambia wameanzisha mradi wa kuwawezesha vijana vijijini kwa kuwapa mafunzo ya ujasiriamali katika kilimo na ufungaji, ikiwa ni mpango wa malengo ya maendeleo endelvu ya mwaka 2030 katika kutokomeza umasikini.

Sauti
44"