Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wadau wa kimataifa watoa wito wa utulivu Garowe Somalia baada ya majeshi kuanza kukusanyika: UNSOM

Mama akimtunza mtoto wake mwenye umri wa miaka 11, ambaye alijeruhiwa na makombora katika shambulio la mabomu, katika hospitali kuu ya Garowe, Somalia mnamo tarehe 27 Februari 2023. (Maktaba)
UN Photo/Fardosa Hussein
Mama akimtunza mtoto wake mwenye umri wa miaka 11, ambaye alijeruhiwa na makombora katika shambulio la mabomu, katika hospitali kuu ya Garowe, Somalia mnamo tarehe 27 Februari 2023. (Maktaba)

Wadau wa kimataifa watoa wito wa utulivu Garowe Somalia baada ya majeshi kuanza kukusanyika: UNSOM

Amani na Usalama

Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia UNSOM kwa ushirilkiano na wadau wengine wa kimataifa wamesema wana wasiwasi mkubwa kuhusu hatari ya mivutano zaidi ikiwemi hali ya sasa ya kukusanya majeji huko Garowe.

UNSOM imesema kukusanyika huko kwa majeshi Garowe kunatisha raia na kumesababisha kufungwa kwa shule.

UNSOM imesisitiza kwamba “Hakuna kinachohalalisha machafuko au tishio la kutumia nguvu. Madai yote yanapaswa kushughulikiwakwa njia ya amani na kupitia majadiliano. Tunatoa wito kwa pande zote kushughilkia tofauti zao kupitia njia za amani”

Taarifa hiyo ya Pamoja imesema wadau wa kimataifa wanaenendelea kuiungamkono na kuisaidia Somalia na watu wake katika kujenga msingi kwa ajili ya amani ya kudumu na mustakbali bora kwa jamii nzima.

UNSOM imesema “Tunaendelea kufuatilia kwa karibu hali na tunatoa wito wa kuacha mivutano mara moja na kuanzisha haraka mazungumzo ya kisiasa  na viongozi wengine wa kijamii.”