Mjumbe wa KM kuonana na viongozi wa Serikali Usomali
Wiki hii Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu kwa Usomali, Ahmedou Ould-Abdallah alifanya ziara ya siku tatu kwenye taifa hilo liliopo Pembe ya Afrika. Alipozuru Baidoa, palipo kikao cha Serikali ya Mpito, Ould-Abdallah alichukua fursa ya kuhutubia bunge.