Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe wa KM kuonana na viongozi wa Serikali Usomali

Mjumbe wa KM kuonana na viongozi wa Serikali Usomali

Wiki hii Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu kwa Usomali, Ahmedou Ould-Abdallah alifanya ziara ya siku tatu kwenye taifa hilo liliopo Pembe ya Afrika. Alipozuru Baidoa, palipo kikao cha Serikali ya Mpito, Ould-Abdallah alichukua fursa ya kuhutubia bunge.