Israel na Palestina: Mkutano mwingine wa dharura wa Baraza la Usalama
Mwishoni mwa juma lililopita, wanajeshi wengi wa nchi kavu wa Israel walipoingia katika Ukanda wa Gaza, hali ya kibinadamu huko Gaza ilikuwa ya wasiwasi. Kwa ombi la China na Umoja wa Falme za Kiarabu, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hivi sasa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani linaendelea na kikao cha dharura kuhusu mzozo huo.