Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wajumbe wakikutana kuhusu hali ya Mashariki ya Kati, likiwemo suala la Palestina.
UN Photo/Eskinder Debebe

Israel na Palestina: Mkutano mwingine wa dharura wa Baraza la Usalama

Mwishoni mwa juma lililopita, wanajeshi wengi wa nchi kavu wa Israel walipoingia katika Ukanda wa Gaza, hali ya kibinadamu huko Gaza ilikuwa ya wasiwasi. Kwa ombi la China na Umoja wa Falme za Kiarabu, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hivi sasa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani linaendelea na kikao cha dharura kuhusu mzozo huo.

UNICEF na Equal Access International, wabuni mbinu za kukabiliana na changamoto katika jamii nchini Kenya. Vijana wahamasishwa kupitia programu za redio.
UNICEF

UNICEF na wadau wake wabuni mbinu za kukabiliana na janga la tabianchi na changamoto katika jamii nchini Kenya

Janga la tabianchi limesababisha kupotea kwa upatikanaji wa elimu, huduma muhimu, na ajira kwa vijana nchini Kenya, hata hivyo Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) nchini humo kwa kushirikiana na shirika la Equal Access International wanawawezesha vijana kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko tabianchi na kutoa ufahamu kuhusu suluhisho la kukabiliana na tatizo hilo. 

Sauti
3'37"
Familia zikikimbia kutoka kwenye makazi ya muda ya Tal al- Hawa kwenda kupata hifadhi Kusini mwa Gaza
© UNICEF/Eyad El Baba

Simulizi wa wajawazito walioko Gaza

Wakati mzozo katika Ukanda wa Gaza ambalo ni eneo la wapalestina linalokaliwa na Israel ukizidi kuongezeka huku wananchi wakikabiliwa na changamoto nyingine lukuki ikiwemo uhaba wa chakula, maji, mafuta na vifaa vya matibabu vya kuokoa maisha, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu na Afya ya Uzazi UNFPA limesema mfumo wa afya nao uko ukingoni kuanguka. Shirika hilo limezungumza na wanawake wajawazito walioko Gaza kuhusu hali mbaya wanayokabiliana nayo. 

Sauti
3'9"
Mfanyakazi wa WFP akipakua misaada ya chakula ambacho kiko tayari kuliwa kutoka kwenye lori kribu na Alexandria Misri tayari kukiingiza Gaza chakula hicho
© WFP/Amira Moussa

Gaza: Maelfu wanavamia maghala ya Umoja wa Mataifa; ishara ya kukata tamaa baada ya mashambulizi ya wiki kadhaa

Mashirika ya misaada yameonya hii leo kwamba utaratibu wa kiraia unaanza kuvunjika huko Gaza baada ya maelfu ya watu waliokata tamaa kuvamia maghala yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa na vituo vingine vya usambazaji wa misaada katika eneo lililoharibiwa, wakichukua unga wa ngano, vifaa vya usafi na bidhaa nyingine muhimu za kujiokoa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia wanahabari mjini Kathmandu, Nepal.
UN Nepal

Hali huko Gaza 'inakuwa ya kukatisha tamaa kila saa', asema Mkuu wa Umoja wa Mataifa 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameanza ziara yake rasmi nchini Nepal kwa kutoa salamu za rambirambi kwa familia za wanafunzi 10 wa Nepal waliouawa katika mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa na Hamas nchini Israel, na kwa mara nyingine tena kutoa wito wa kulindwa kwa raia wote huko Gaza akisema, “hali inakua ya kukatisha tamaa kila saa.”