Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwanamke akishiriki katika maandamano ya kupinga ukatili wa kijinsia huko Quito, Ecuador.
© UN Women/Johis Alarcón

Wanawake na wasichana ndio walio hatarini zaidi kuuawa majumbani: UN Women/UNODC

Ripoti ya utafiti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNODC inaonyesha kuwa wanawake na wasichana ndio walio katika hatari kubwa ya kuuawa majumbani, ikionyesha kuwa kwa wastani zaidi ya wanawake au wasichana watano waliuawa kila saa na wenzi wao au jamaa wa familia kwa mwaka 2021. 

Sauti
3'33"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia Mkutano wa 9 wa Kimataifa wa Muungano wa Ustaarabu wa Umoja wa Mataifa huko Fez, Morocco.
UN News/Alban Mendes De Leon

Tuanzishe ‘ushirika wa amani’ ili kila mtu aishi kwa utu na apate fursa- Guterres

Katika dunia ambayo “maovu ya zamani – chuki dhidi ya wayahudi, ubaguzi dhidi ya wasio waislamu, utesaji wa wakristo, chuki dhidi ya wageni na ubaguzi – vinaendelea kupatiwa tena uhai,” amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres huku akiongeza kuwa Jukwaa la Umoja wa Mataifa la Ustaarabu, UNAOC linasaidia kuonesha njia ya jinsi ya kuchukua hatua kwa mshikamano. 

Tuzo ya mazingira ya UNEP 2022 yawaenzi warejesha mifumo ya ikolojia
UNEP/Duncan Moore

Tuzo ya mazingira ya UNEP 2022 yawaenzi warejesha mifumo ya ikolojia

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP leo limetangaza washindi wa tuzo yake kubwa kabisa ya mazingira Champion of the Earth 2022 ikiwaenzi mhifadhi wa mazingira, mfanyabiashara, mwanauchumi, mwanaharakati wa haki za wanawake, na mwanabiolojia wa wanyamapori kwa hatua zao za kuleta mabadiliko ya kuzuia, kusitisha na kubadili uharibifu wa mfumo ikolojia.