Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Bi. Salma Mukansanga, Mchechemuzi wa UNICEF kwa kipindi cha miezi 12 ili kusaidia utekelezaji wa Mkakati wa Uchechemuzi chini ya UNICEF Rwanda.
©UNICEF/Steve Nzaramba

Salima Mukansanga - Kama mimi nimefika Kombe la Dunia, hakuna ambako huwezi kufika

Michuano ya fainali za Kombe la Dunia kwa mchezo wa soka kwa wanaume inaendelea nchini Qatar huko Mashariki ya Kati. Mmoja wa watu wanaong’ara katika michuano hii ni Mchechemuzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Rwanda, Salima Mukansanga, ambaye ameweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi kuwa mwamuzi au refarii katika Kombe la Dunia. Aliingiaje katika tasnia hii ya mpira wa miguu? UNICEF Rwanda ilizungumza naye kabla hajasafiri kwenda Qatar na hapa Anold Kayanda anaeleza kwa lugha ya Kiswahili kilichozungumzwa. 

Sauti
2'39"
Virusi vya ndui ya nyani vinaweza kusambazwa kupitia malengelenge
© Harun Tulunay

Monkeypox au Ndui ya Nyani yabadilishwa jina sasa kutambulika MPOX

Baada ya mfululizo wa mashauriano na wataalamu wa kimataifa, hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO litaanza kutumia jina MPOX badala ya Monkeypox au homa ya Ndui ya Nyani kufuatia mapendekezo ya kubadilishwa kwa jina hilo kwa maelezo ya kwamba lilikuwa linasababisha mambo kadhaa ikiwemo unyanyapaa. 

Sauti
2'24"