Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mkimbizi akibeba chakula mgao uliotolewa na WFP katika kituo kambi ya Kakumba nchini Kenya.
WFP

WFP nchini Kenya yapokea ufadhili mkubwa zaidi wa kupambana na njaa 

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limekaribisha mchango wa dola za Marekani milioni 194.5 kutoka kwa Serikali ya Marekani, kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), ili kutoa msaada muhimu wa chakula na lishe na kujenga uwezo wa kukabiliana na hali hiyo kwa maelfu ya watu wanaokabiliwa na changamoto za ukame mbaya zaidi katika miongo minne.  

Watoto hawa wa shule katika shule ya msingi ya Naipa kaunti ya Turkana nchini Kenya. Wako hatarini kukumbwa na ndoa kwenye umri mdogo.
© UNICEF/UNI3Andrew Brown

Ukame umeniponza nusura niozwe kwa mzee: Carol

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema watoto wengi na hususan wa kike katika jamii zilizoathirika na ukame nchini Kenya ikiwemo Turkana wako katika hatari  hasa ya kuozwa mapema kwa sababu familia nyingi zinahaha kuweka mlo mezani na suluhu ya karibu wanayoiona ni kuoza binti zao mapema ili kujikimu. Sasa shirika hilo linashirikiana na mamlaka za huduma ya ulinzi kwa watoto katika maeneo yaliyoathirika ili kuwalinda dhidi ya ajira ndoa za utotoni. 

Sauti
3'35"