Mali tuko mwelekeo sawa wa mpito unaokoma Machi 2024- Kanali Maiga
Katika siku ya tano ya Mjadala Mkuu wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 jijini New York, Marekani, Mali imesema iko kwenye mwelekeo sahihi wa kipindi cha serikali ya mpito kilichoanza mwezi Agosti mwaka 2020 na ukomo wake mwezi Machi mwaka 2024.