FAO Tanzania yazindua mradi wa zaidi ya dola milioni 9 kuimarisha mimea na usalama wa chakula
Katika kutekeleza lengo namba 15 la Maendeleo endelevu kuhusu kuimarisha uhai wa viumbe vya nchi kavu Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) kwa kushirikiana na Muungano wa Ulaya, (EU) limezindua mradi wa kuimarisha Huduma za Afya ya Mimea na usalama wa chakula nchini Tanzania.