Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hema katika jangwa nchini Mauritania
Unsplash / Daniel Born

Sasa hatuna wasiwasi tena mvua isiponyesha:Wakulima Mauritania

Mabadiliko ya tabianchi yanaleta madhara kila kona ya dunia ikiwemo kupungua kwa viwango vya mvua na hivyo kuleta usumbufu mkubwa wa wakulima, mathalan nchini Mauritani kiwango cha mvua kilichokuwa kikinyesha miaka 30 iliyopita sasa wanapata robo tu ya kiwango hicho hali iliyowatesa wakulima na wafugaji lakini mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo IFAD umewanusuru kwa kuwahakikishia maji mwaka mzima.

Sauti
2'23"
Mwandishi wa habari raia wa Urusi Dmitry Muratov na mshindi wa tuzo ya Nobel
UN News/Nargiz Shekinskaya

Tuzo ya mshindi wa Nobel yauzwa dola milioni 103.5 fedha kugawanywa na UNICEF

Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Dmitry Muratov ambaye alipiga mnada medali yake ya dhahabu ili kuchangisha fedha kwa ajili ya wakimbizi watoto Juni 20, 2022 ameiambia Idhaa ya Umoja wa Mataifa kwamba Kitendo cha medali yake kuvunja rekodi kwa kuuzwa dola milioni 103.5 kimethibitisha kwamba "wakati mwingine ubinadamu unaweza kuja pamoja, na kuoyesha mshikamano".

Mtoto majeruhi wa tetemeko la ardhi nchini Afghanistan akipata matibabu katika hospitali ya wilaya ya Urgun.
© UNICEF Afghanistan

Mamia ya watu wapoteza maisha kwenye tetemeko la ardhi Afghanistan UN yajipanga kusaidia

Wadau wa kimataifa wa misaada ya kibinadmu yakiwemo mashirika ya Umoja wa Mataifa wanajiandaa kusaidia maelfu ya familia zilizoathirika zaidi na tetemeko kubwa la ardhi lililokubwa majimbo ya Paktika na Khost nchini Afghanistan mapema leo, mamia ya watu wameripotiwa kufariki dunia, wengi kujerihiwa wengine vibaya sana huku miundombinu ikiharibiwa vibaya.

Sauti
2'16"