Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kijana akionesha mikono yake wakati wa mlipuko wa monkeypox DRC.(Maktaba)
CDC

Monkeypox ni tishio lakini si dharura ya afya ya umma inayoleta hofu ya kimataifa: WHO

Ingawa mlipuko wan dui ya nyani au monkeypox unaendelea na umeshasambaa katika mataifa kadhaa ulimwenguni mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema “Nina wasiwasi mkubwa na kusambaa kwa mlipuko wa monkeypox ambao ni tishio linaloendelea, nimeitisha kikao cha kamati ya dharura ya WHO, na wataalam wameshauri kwamba kwa sasa ugonjwa huo sio dharura ya afya ya umma inayotia hofu ya kimataifa.”