Kongamano la 11 la mijini duniani limeng’oa nanga Katowice, Poland:UNHABITAT
Kikao cha kumi na moja cha Kongamano la kimataifa la miji endeleu kimefunguliwa rasmi leo Katowice, Poland kwa wito wa kuongeza juhudi maradufu ili kukabiliana na changamoto zinazoletwa mijini na janga la COVID-19, dharura ya mabadiliko ya tabianchi na migogoro.