Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kapteni Abdelrazakh(katikati) alitumwa kambi ya wakimbizi ya Aguelhok Kaskazini mwa Mali wakati ilishambuliwa na kundi la kigaidi.
Kwa hisani ya Luteni Kanali Chahata Ali Mahamat

Mwendazake Kapteni Abdelrazakh Hamit Bahar wa Chad ashinda tuzo ya pili ya UN ya kulinda amani kwa 'ujasiri wa kipekee' 

Marehemu Kapteni Abdelrazakh Hamit Bahar wa Chad, alitajwa Jumanne ya wiki hii kama mpokeaji wa tuzo ya juu zaidi ya Umoja wa Mataifa ya Kulinda Amani, kwa ujasiri wa kipekee, akihudumu nchini Mali, ambayo itatolewa Alhamisi hii katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa  New York, Marekani. 

Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet mkutanoni kwa njia ya mtandao na rais wa China Xi Jinping ziarani Guangzhou, China.
© OHCHR

Bachelet afanya mikutano ya muhimu na Rais Xi wa China 

Katika siku ya tatu ya ziara yake rasmi nchini China, kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amelezea kuwa ni fursa muhimu ya kuangazia masuala ya haki za binadamu na shuku na shaka katika mazungumzo yake na Rais Xi Jinping na maafisa wengine wakuu wa serikali , ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina hiyo kufanywa na mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa tangu mwaka 2005. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres atunukiwa shahada ya heshima kutoka Chuo Kikuu cha Seton Hall kilichopo New Jersey nchini Marekani.
UN Photo/Evan Schneider

Msifanye kazi kwa waharibifu wa mazingira : Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia wanafunzi wanaohitimu katika Chuo Kikuu cha Seton Hall kilichoko Newark, New Jersey, nchini Marekani  amewaambia “kutofanya kazi kwa waharibifu wa tabianchi” na badala yake watumie talanta zao “kusukuma kuelekea mustakabali unaoweza kurejesha uharibifu uliofanyika.”

Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt. Tedros Ghebreyesus akizungumza katika moja ya taarifa za WHO kuhusu janga la COVID-19
UN Photo/Evan Schneider

Dkt. Tedros kuiongoza WHO kwa awamu ya pili

Mkutano Mkuu wa 75 wa nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO uliofanyika leo jijini Geneva Uswisi umemthibitisha Dkt.Tedros Adhanom Ghebreyesus kuliongoza shirika hilo kwa awamu ya pili ya miaka 5.