Kila mtu anapaswa kulindwa kwa tahadhari ya mapema dhidi ya majanga:UN
Ikiwa leo ni siku ya utabiri wa hali ya hewa duniani, malengo mapya ya Umoja wa Mataifa yalioyotangazwa leo yanataka katika miaka mitano ijayo kila mtu kote duniani alindwe kwa kupewa tahadhari ya mapema dhidi ya ongezeko la hali mbaya ya hewa na mabadiliko ya tabianchi.