Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Familia ya raia wa Burundi mbele ya nyumba yao iliyoharibiwa na kimbunga Gombe, katika makazi ya wakimbizi ya Maratane, Msumbiji.
© UNHCR/Juliana Ghazi

Kimbunga Gombe, Msumbiji, UNHCR na wadau wanaharakisha msaada kwa maelfu

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR pamoja na serikali ya Msumbiji na washirika wa kibinadamu, wanaharakisha kusaidia maelfu ya familia zilizoathiriwa na kimbunga cha Tropiki cha Gombe, ambacho kilipiga katika jimbo la Nampula mnamo tarehe 11 ya mwezi huu wa Machi na kuharibu nyumba, maji kufunika mashamba, na kuwalazimisha watu kuyakimbia makazi yao ili kutafuta usalama.   

Mwanaume akipima VVU kwenye kituo kimoja cha afya huko Odienné, nchini Côte d’Ivoire.
© UNICEF/Frank Dejongh

Sindano mpya ya Cabotegravir kusaidia kukinga wengi dhidi ya  VVU:UNITAID 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa za tiba kwa gharama nafuu, UNITAID limetangaza utekelezaji wa mchakato mkubwa wa uvumbuzi wa hivi karibuni katika kuzuia virusi vya ukimwi ,VVU ambao ni sindano mpya  ambayo inachukua wiki nane kabla ya muathirika kupewa dozi nyingine badala ya tembe anazopaswa kumeza kila siku.

Sauti
2'25"