Guterres aunga mkono maandalizi ya azimio la kupinga vilipuzi
Huko Geneva, Uswisi kuanzia tarehe 6 hadi 8 ya mwezi ujao wa Aprili kunafanyika mashauriano yasiyo rasmi yenye lengo la kuandaa azimio la kisiasa la kulinda raia dhidi ya matumizi ya vilipuzi katika maeneo ya makazi ya watu wengi.