UN yatiwa hofu na ripoti za kushikiliwa kwa Rais wa Burkina Faso
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ana wasiwasi mkubwa kuhusu mahali aliko na usalama wa Rais wa Burkina Faso Roch Marc Christian Kaboré.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ana wasiwasi mkubwa kuhusu mahali aliko na usalama wa Rais wa Burkina Faso Roch Marc Christian Kaboré.
Ikiwa leo ni siku ya elimu duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la COVID-19 na changamoto nyingine zinazokabili Dunia hivi sasa zimedhihirisha umuhimu wa kurekebisha mfumo wa elimu ili uweze kukidhi mahitaji ya sasa.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF limesema kiwango cha hasara wanayopata watoto kielimu kutokana na kuvurugika kwa mfumo wa elimu kulikosababishwa na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 ni vigumu kurekebishika.
Takribani watoto milioni 1.5 katika maeneo ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, hawapati matibabu ya kuokoa maisha kutokana na uzito mdogo ikilinganishwa na urefu wao, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limeonya leo.
Hii leo Januari 21, mwaka 2022, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewasilisha vipaumbele vyake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya ngwe nyingine ya mwaka baada ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaja mambo makuu matano anayoona yanapaswa kupatiwa kipaumbele ili dunia iweze kuwa na mwelekeo sahihi na mustakabali bora kwa kila mkazi wake.
Timu ya wanasayansi iliyokuwa imetumwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni kufanya utafiti baharini imebaini moja ya miamba nadra na kubwa zaidi wa matumbawe karibu na Tahiti huko bahari ya Pasifiki.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio ambalo linalaani ukataaji na upindishaji wa suala la mauaji ya halaiki au holocaust.
Kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa wimbi la nne la COVID-19 barani Afrika linalochochewa na virusi aina ya Omnicron, idadi ya maambukizi mapya imepungua na hivyo kuashiria kupungua kwa idadi ya vifo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo amesema juhudi za vijana za kujenga na kusongesha amani bado hazijawa na mchango unaotakiwa kwa sababu hawajashirikishwa kwa kina kwenye meza ya mazungumzo.