Wanawake wengi sana wanaendelea kufa kutokana na utoaji mimba usio salama: WHO
Wasichana na wanawake wengi sana wanaendelea kufa na kukabiliwa na matokeo mabaya ya uavyaji mimba usio salama, hata hivyo kuna ukosefu wa taarifa kuhusu jinsi huduma bora inaweza kutolewa kwa wasichana na wanawake wenye matatizo yanayohusiana na utoaji mimba, limesema Shirika la Afya Ulimwenguni la Umoja wa Mataifa, WHO.