Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Muhudumu wa afya akimuhudumia mgonjwa katika ukumbi uliobadilishwa matumizi na kuwa wodi ya muda ya wagonjwa wa COVID-19 huko New Delhi, India
© UNICEF/Amarjeet Singh

WHO yatoa wito wa watoa hudumu ya afya kulindwa dhidi ya COVID-19

wafanyikazi wa huduma za afya kwa jumla wamelipa gharama kubwa wakati wa janga la COVID-19. Na shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani (WHO) na washirika wake leo mjini Geneva Uswis wamezindua ombi la dharura la kuchukua hatua madhubuti ili kulinda vyema afya na wahudumu wa afya kote ulimwenguni dhidi ya virusi vya Corona na changamoto zingine za kiafya.

Katibu Mkuu  António Guterres ametembelea maonesho ya picha ya "Mikononi mwao: Wanawake wachukua umiliko wa amani" katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
UN Photo/Mark Garten)

Muda wa kurudisha nyuma saa ya haki za wanawake umepita, sasa iende mbele- Guterres alieleza Baraza

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu wanawake, amani na usalama ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakati umefika kwa baraza hilo kuonesha kwa vitendo uungaji wake mkono wa harakati za wanawake katika ujenzi na uendelezaji wa amani badala ya kusalia maneno matupu.  Flora Nducha na maelezo zaidi.

Sauti
3'18"