Madagascar: Njaa kali inayochochewa na mabadiliko ya tabianchi?
Zaidi ya watu milioni moja kusini mwa Madagascar wanahaha kupata mlo, nah ii inaweza kuwa ni tukio la kwanza kabisa duniani la watu kukumbwa na njaa kutokana na mabadiliko ya tabianchi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP.