Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Imani Nsamila (wa nne nyuma kutoka kushoto) akiwa na kundi la wasichana waliohudhuria warsha ya upigaji picha.
UN/Imani Nsamila

Tumedhamiria kupunguza pengo la kijinsia katika tasnia ya upigaji picha Tanzania-Nsamila

Nchini Tanzania, mpiga picha maarufu, Imani Nsamila, kwa kushirikiana na shirika la Ladies Joint Forum na Kikoi innovative media, wamewapa mafunzo ya upigaji picha wasichana 28 ikiwa ni moja ya harakati za kuchangiakuyafikia malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs, kama vile lengo namba 5 linalolenga ulimwengu kuwa na usawa wa kijinsia kufikia mwaka 2030. 

Sauti
3'24"
Mwanafunzi wa shule ya msingi akisoma nyumbani kwao Kibera, Kenya.
© UNICEF/Brian Otieno

WHO, UNICEF zataka shule zifunguliwe kwa njia salama Afrika

Mashirika ya Umoja wa Mataifa la afya WHO na la kuhudumia watoto UNICEF yamesema hatua ya shule kufungwa kwa muda mrefu kwa lengo la kuwalinda wanafunzi na virus vya corona au COVID-19 inawaumiza wanafunzi hao kwa njia nyingine na wamezitaka serikali barani Afrika kuchaguza ufuanguaji salama wa shule huku zikichukua hatua kudhibiti maambukizi ya virusi hivyo. 

Sauti
3'1"