Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kundi la nzige likiwa angani kwenye moja ya mashamba
© FAO/Giampiero Diana

Kama nzige hawa hawataisha na mvua ikanyesha japo kiasi, mifugo yetu itakufa- Wafugaji Turkana

Hivi karibuni tulikueleza namna ambavyo nzige wavamizi wa jangwani wanavyotishia ustawi wa wakulima wa Kenya hususani  katika  eneo la Turkana, lakini kwa mujibu wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa mataifa FAO, nzige hao hawaishii tu katika kilimo bali pia wanatishia jamii ya wafugaji kwani wanakula hadi nyasi na miti ambayo ingekuwa chakula cha kifugo.

Sauti
2'50"
Hilda Phoya, mnufaika wa mafunzo kwa vitendo katika ofisi za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania.
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Umoja wa Mataifa una fursa nyingi, muhimu vijana tuwe tayari na tuwe na moyo wa kujitolea-Hilda Phoya

“Umoja wa Mataifa una fursa nyingi ambazo ikiwa vijana tutakuwa na moyo wa kujitolea na bidii ya kazi, tunaweza kunufaika nazo,” hayo ni maoni ya Hilda Phoya, mwanafunzi ambaye hivi karibuni amehitimisha mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha habari za Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam Tanzania. 

Sauti
3'7"