Mlipuko wa Ebola mashariki mwa DRC umetokomezwa, WHO yapongeza
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imetangaza kutokomezwa kwa mlipuko wa 10 wa Ebola mashariki mwa nchi hiyo ulioanza mwezi Agosti mwaka 2018.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imetangaza kutokomezwa kwa mlipuko wa 10 wa Ebola mashariki mwa nchi hiyo ulioanza mwezi Agosti mwaka 2018.
Ikiwa leo ni siku ya mabaharia duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema kuwa sasa ni wakati muafaka wa kuwapa mabaharia heshima wanayoistahili.
Nchini Sudan Kusini, ujumbe wa Umoja wa Mataifa UNMISS umewaondolewa wanafunzi wa eneo moja mjini Yambio jimboni Equitoria Magharibi adha ya kusomea chini ya mti kwa kuwajengea madarasa ambamo watasomea bila bughudha yoyote
Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, nchi waangalizi na wengineo wametuma ujumbe mzito wa kisiasa wiki hii kwa kutangaza kwamba sahihi 170 sasa zimeidhinisha wito wa Umoja wa Mataifa wa kunyamazisha silaha na kusimama Pamoja dhidi ya tishio la kimataifa la janga la virusi vya corona au CIVID-19.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza kwa njia ya video kwenye Baraza la Usalama hii leo ametoa wito kwa Israel na kuisihi kutotekeleza mipango yake ya upanuzi wa makazi ya walowezi kwenye Ukingo wa Magharibi.
Ripoti mpya ya fuko la kimataifa la ufadhili Global Fund iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi inakadiria kuwa nchi ambazo zimeathirika na Virusi Vya UKIMWI, VVU, Kifua Kikuu yaani TB na Malaria, kwa haraka zinahitaji dola bilioni 28.5 za kimarekani ili kulinda hatua kubwa zilizokwisha kufikiwa katika miongo miwili iliyopita katika mapambano dhidi ya magonjwa hayo matatu.
Ni saa tatu asubuhi jua limeshaanza kutoa miale yake katika makazi ya wakimbiziya Bidibidi katika Wilaya ya Yumbe nchini Uganda. Wanawake wamekusanyikakaribu na kisima cha maji ili kuchota maji ya asubuhi halafu watarudi tena papa hapa jioni.
Kipaji na mapenzi ya uchoraji wa sanaa vimempatia mkimbizi kutoka Eritrea anayeishi nchini Libya faraja na matumaini wakati huu wa zama za janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, linalogubikwa pia na mapigano na kudorora kwa hali ya kiuchumi na kijamii katika taifa hilo la Afrika Kaskazini.
Nchini Tanzania hospitali ya CCBRT imechukua hatua za uhakika kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu, wakiwemo wafanyakazi wake wanajikinga ipasavyo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
Katiba ya Umoja wa Mataifa ikiwa inaelekea kutimiza miaka 75 juma hili Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterrres amesema changamoto lukuki zinazoikabili dunia hivi sasa zinahitaji mwongozo ili kuzitatua na mwongozo huo ni katiba ya Umoja wa Mataifa.