Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Madaktari wakifurahi baada ya mgonjwa kupona kutoka hali mahututi kufuatia maambukizi ya ugonjwa wa corona.
Department of Critical Care Medicine, Affiliated Hospital of Guangdong Medical University

Ondoeni vikwazo kusaidia COVID-19, madaktari wasemao ukweli msiwaadhibu- Bachelet

Wakati idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 ulimwenguni ikizidi kupaa na kuwa zaidi ya 330,000 huku vifo vikifikia 14,652 Kamishna Mkuu wa haki za binadamu, Michelle Bachelet ametaka vikwazo vya kisekta duniani viondolewe ili mataifa yaweza kukabiliana na mlipuko wa virusi hivyo.

Sauti
2'7"
Hospitali ya CCBRT nchini Tanzania
UN News/ UNIC Tanzania

Wafanyakazi wenye ulemavu CCBRT Tanzania wapatiwa mafunzo ya dhidi ya COVID-19

Nchini Tanzania mafunzo kuhusu virusi vya Corona na jinsi ya kukabiliana navyo ambayo yanatolewa kwa watendaji wenye ulemavu katika hospitali ya CCBRT yemekuwa na manufaa makubwa wakati huu ambapo tayari taifa hilo la Afrika Mashariki limethibitisha kuwa na wagonjwa wa virusi hivyo. Ni kwa vipi basi? Tuungane na Hilda Phoya mwanafunzi anayefanya mafunzo kwa vitendo katika kituo cha habari za Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam ambaye amevinjari katika hospitali hiyo.

Sauti
2'13"
Kijiji nchini Sudan Kusini, barabarani kati ya Yambio na Maridi, Equatoria ya Magharibi.
UN Photo/JC McIlwaine

Kamwe sitakata tamaa. Nitashinda!-Nakout Slylvia

Nakout Sylvia alitekwa nyara na kikundi cha waasi cha Uganda mnamo 2003 na alikamatwa mateka kwa miaka 12 huko Afrika ya Kati. Kama matokeo ya unyanyasaji wa kijinsia wa kila mara, aliambukizwa Virusi Vya UKIMWI, VVU. Nakout baadaye alifanikiwa kutoroka na akapata hifadhi nchini Finland ambako sasa ameanza kujifunza mchezo wa gofu wa frisbee ambao ni maarufu nchini Finland. Je maisha yake hivi sasa yako vipi?

Sauti
2'19"