Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Leo nchini Chad kuna takriban watu 657,000 waliofurushwa makwao asilimia 51 ni wanawake na wasichana.
OCHA/Naomi Frerotte

Migogoro ya kijamii nchini Chad yawalazimisha watu 8,300 kukimbilia Darfur

Zaidi ya watu 6000 nchini Chad, wakwiemo  wanaume, wanawake na watoto wamekimbilia katika mji wa Tina na Karnoi huko Kaskazini mwa Darfur Sudan kutokana na mapigano kati ya makundi tofauti ya kabila la Zaghawa katika eneo la Tina, upande wa pili wa mpaka nchini Chad, imeeleza taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR iliyochapishwa hii leo.

Sauti
1'48"