Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Vijana wa kiume wakitizama soka kupitia televisheni Volta Redonda, Brazil.
Unsplash/Gustavo Ferreira

Televisheni haifi ng’o!- ITU

Ikiwa leo ni siku ya televisheni duniani, shirika la mawasiliano la Umoja wa Mataifa, ITU limesema chombo hicho cha mawasiliano kitaendelea kuwa na umuhimu mkubwa katika kuongeza uelewa wa masuala ya mambo miongoni mwa binadamu.

Rangi ya buluu iliangaza ndani ya ukumbi wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto, CRC.
UN Photo/Manuel Elías

Rangi ya buluu ikitawala, Beckham asema "siku zijazo ni za watoto wetu hivyo tutunze ndoto zao"

Mustakabali si wa kwetu bali ni wa watoto wetu kwa hiyo tuchukue hatua zaidi kulinda ndoto za watoto, amesema David Beckham, Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, wakati akihutubia hii leo kikao cha ngazi  ya  juu cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kilichofanyika kuadhimisha miaka 30 tangu kupitishwa kwa mkataba wa haki za mtoto, CRC na sambamba na siku ya mtoto duniani,

 

Makazi ya Walowezi wa Kiyahudi ya Har Gilo kwenye Ukingo wa Magharibi karibu na Jerusalem
Photo: IRIN/Erica Silverman

Hali bado iko njia panda kati ya Israeli na kundi la Kipalestina-Mladenov

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo Jumatano limekutana kujadili suala la Mashariki ya Kati ambapo mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati Nickolay Mladenov ameonya kwamba kikao hicho kinafanyika baada ya kushuhudiwa ongezeko la machafuko kati ya Israeli na kundi la Kipalestina la Islamic Jihad huko Gaza.