Teknolojia ya kidijitali ndio mwelekeo sasa, twende nayo sambamba:Guterres
Teknolojia ya dijitali ndio inayounda dunia hivi sasa na inakwenda kwa kasi isiyo ya kawaida hivyo kila mtu katika dunia hii anapaswa kwenda na kasi hiyo, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo.