Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtambo wa makaa ya mawe Tuzla, Bosnia
UNEP

Bila kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kwa asilimia 7.6 lengo la nyuzi joto 1.5 halitafikiwa-Ripoti ya UNEP

Katika kuelekea mwaka ambao mataifa yataimarisha ahadi zao za ulindaji wa hali ya hewa zilizoafikiwa mjini Paris, ripoti mpya iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP, imeonya kuwa, ulimwengu utashindwa kufikia lengo la nyuzi joto 1.5 la mkataba wa Paris ikiwa dunia haitapunguza hewa chafuzi kwa asilimia 7.6 kila mwaka kati ya mwaka 2020 na 2030.

Mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya ukimwi Winnie Byanyima (wa pili Kushoto) katika uzinduzi wa Ripoti ya Ukimwi mjini Thika nchini Kenya
UN AIDS

Pengo la usawa ndio mtihani wetu katika vita dhidi ya UKIMWI:UNAIDS

Jumla watu milioni 24.6 walikuwa wanapata matibabu dhidi ya virusi vya UKIMWI, VVU,  hadi Juni mwaka 2019 kwa mujibu wa ripoti mpya ya  ya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya UKIMWI, UNAIDS iliyiozindulwa hii leo nchini Kenya. Hata hiyo ripoti hiyo inasema kuwa watu milioni 32 wamepoteza maisha kote dunia tangu ugonjwa huo ugunduliwe. 

Sauti
2'19"
Wingu katika eneo la Plechotice, Slovakia
WMO/Monika Nováková

Ripoti ya WMO yabaini ongezeko la hewa chafuzi katika anga

Ripoti ya shirika la hali ya hewa duniani WMO iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi imeonesha ongezeko zaidi la hewa chafuzi katika anga. Hali hii inayoendelea kwa muda mrefu  inaamaanisha kuwa vizazi vijavyo vitakabiliana na ongezeko la matokeo mabaya ya mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ongezeko la joto, mabadiliko makubwa ya hali uya hewa, upungufu wa maji, kuongezeka kwa kina cha bahari na uharibifu kwa viumbe wa majini na ardhini.