Bomu la kurushwa kutoka angani linahofiwa kuua wengi Yemen
Taarifa ya pamoja iliyotolewa hii leo jumapili mjini Sana’a na mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen pamoja na mwakilishi mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini humo imeeleza kuwa taarifa za awali zinaonesha kuwa takribani watu 60 wamefariki na wengine 50 kujeruhiwa katika eneo lililoko kaskazini mwa viunga vya mji wa Dhamar kwenye eneo ambalo awali lilikuwa chuo lakini sasa likitumika kama gereza linalokadiriwa kuwa na wafungwa 170.