Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Melissa Fleming (kushoto) alipokuwa msemaji na mkuu wa mawasiliano wa UNHCR, akimuhoji Fabrizio Hochschild, msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya mikakati na uratibu.
UNHCR/Susan Hopper

Melisa Fleming ndio mkuu mpya wa idara ya mawasiliano ya kimataifa UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo amemteua Melissa Fleming raia wa Marekani kuwa ndio mkuu mpya wa idara ya mawasiliano ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa au DGC. Bi. Fleming anachukua wadhifa huo wa msaidizi wa Katibu mkuu akimrithi Alison Smale raia wa Uingereza ambaye Katibu Mkuu amemshukuru kwa uwajibikaji wake na huduma kwenye shirika la Umoja wa Mataifa.

Msichana wa umri wa miaka saba asimama mbele ya jengo la shule lililoharibiwa  mjini Idlib Syria.
UNICEF

UN yaunda kamati kuchunguza matukio ya Idlib Syria

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameamua kuunda kamati ya uchunguzi ili kutathimini mfululizo wa matukio yaliyofanyika Kaskazini Magharibi mwa Syria tangu kutiwa saini makubaliano ya kurejesha utuli wa hali ya taifa hilo la Mashariki ya Kati kwenye eneo la Idlib baina ya Urusi na Uturuki mnamo 17 Septemba 2018.