Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wafanyakazi wa ujenzi katika kituo cha kuzalisha umeme wa maji cha Trung Son Vietnam
World Bank/Mai Ky

Msongo utokanao na ongezeko la joto utasababisha hasara sawa na kazi milioni 80 ifikapo mwaka 2030-“ILO

Makadirio kwa kuzingatia ongezeko la joto la dunia la nyuzi joto 1.5 kufikia mwishoni mwa karne hii yanaonesha kuwa kufika mwaka 2030, asilimilia 2.2 ya jumla ya muda wa saa za kazi kote duniani itapotea kutokana na joto kali, na ni hasara sawa na nafasi za kazi milioni 80.  Maelezo zaidi na Patrick Newma

 

Sauti
2'31"
Wachechemuzi wa malengo endelevu, SDGs yaliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa 2015
UN SDGs

Tunakusudia kuyapandisha malengo ya maendeleo endelevu kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro-Munyaradzi Muzenda

Ikiwa imesalia miaka 11 kuelekea mwaka 2030 ambao ndiyo umepangwa na Umoja wa Mataifa kuwa mwaka ambao malengo ya maendeleo endelevu, SDGs yatakuwa yametimizwa, Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wameendelea kuhamasisha umma kwanza kuyafahamu malengo yenyewe na pia kuyatekeleza. Miongoni mwa wadau hao ni Munyaradzi Muzenda kutoka Zimbabwe ambaye ni mkurugenzi wa taasisi ya Africa Speaks, yeye anaendesha kampeni ya kukuza uelewa kuhusu SDGs, Arnold Kayanda na maelezo zaidi.

Sauti
2'8"