Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanafunzi wakiwa na furaha kwamba darasa  mpya inajengwa shuleni mwao Sakassou mji wa kati wa Côte d'Ivoire kwa kutumia matofali yatoakanyo na taka za plastiki.
UNICEF/Frank Dejo

Muarobaini wa adha ya madarasa Côte d'Ivoire ni taka za plastiki:UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na kampuni ya biashara ya kijamii ya Colombia Conceptos Plasticos, leo wametangaza kuzindua kiwanda cha kwanza cha aina yake ambacho kitabadilisha taka za plastiki zilizokusanywa nchini Cote d'Ivoire na kuzifanya kuwa matofali ya kawaida ya plastiki ya gharama nafuu na yanayodumu kwa muda mrefu, ambayo yatatumika kujenga vyumba vya madarasa vinavyohitajika sana katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Sauti
2'48"
Mahojiano na Wevyn Muganda, Meneja Programu wa Haki Afrika
UN News/Assumpta Massoi

Blogu ya Beyond the Lines yawezesha vijana kuelewa SDG 16

Mwanaharakati wa haki za binadamu kutoka Kenya ambaye pia ni afisa programu wa shirika la kiraia la Haki Afrika Wevyn Muganda amezungumzia vile ambavyo blogu yake ya Beyond the Lines inasaidia kuwezesha vijana kusoma taarifa mbalimbali bila ugumu wowote na hivyo kufanikisha leng namba 16 la maendeleo endelevu, SDGs kuhusu amani,  haki na taasisi thabiti.

Sauti
2'12"