BTS yatoa video maalum, “saka upendo ndani yako uweze kusambaza kwa wengine”
Wanamuziki vijana wa kikundi mashuhuri cha muziki duniani, BTS ambao pia ni waungaji mkono wa kazi za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF wametoa wito kwa vijana kueneza wema katika siku hii ya leo ya kimataifa ya urafiki.