Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wakati vita ilipoanza nchini Yemen mwaka 2015, Yemen ilikuwa imeshawekwa katika kundi la nchi maskini zaidi duniani.
WFP/Reem Nada

Bila fedha mamilioni ya walio na njaa Yemen watakuwa njia panda:WFP

Wakati mkutano wa kimataifa wa uchangishaji fedha kwa ajili ya Yemen ukifanyika leo mjini Geneva Uswis na kuwaleta pamoja wadau mbalimbali  wa kimataifa na mashirika wahisani, shirika la Umoja wa  Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP, limesema linahitaji haraka dola milioni 570 ili kususuru maisha ya mamilioni ya wanaohitaji msaada wa chakula. 

Sauti
2'55"
Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres na Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela Jorge Arreaza
UN / Evan Schneider

Mamlaka Venezuela msitumie silaha za sumu dhidi ya waandamanaji- Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo amekuwa na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela, Jorge Arreaza, ambapo amesisitiza tena kuwa hatua zozote ambazo chombo hicho kitachukua kusaidia wahitaji nchini Venezuela zitazingatia kanuni na misingi ya kibinadamu, kutoegemea upande wowote na mamlaka za taifa hilo na kushirikiana na taasisi za taifa hilo.