Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanafunzi wakiangalia jedwali la elementi au Periodic Table katika shule ya wasichana huko Herat, Afghanistan.
Graham Crouch/World Bank

Jedwali la elementi latimiza miaka 150, UN yapongeza maadhimisho hayo

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO,  leo limezindua mwaka wa kimataifa wa jedwali la elementi kwa kiingereza Periodic Table katika makao yake makuu mjini Paris Ufaransa, ukiwa ni mwanzo wa mfululizo wa matukio na shughuli mbalimbali zitakazofanyika kwa mwaka mzima, wakati dunia ikiadhimisha miaka 150 tangu kuundwa kwa jedwali hilo na mwanasaynsi wa Urusi Dimtri Mendeleev.

Mtoto mkimbizi akiwa mbele ya hema lake katika kisiwa cha Lesvos Ugiriki
UNICEF/UN0274758/Haviv VII

UNICEF yatoa ombi la dola bilioni 3.9 kwa ajili ya kusaidia watoto milioni 41 duniani

Mamilioni ya watoto wanaoishi katika nchi zilizoathiriwa na mizozo na majanga wanakosa huduma muhimu za ulinzi na hiyvo kuweka usalama na mustakabali wao hatarini, limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudmia watoto, UNICEF huku likisema linahitaji ombi la dola bilioni 3.9 ili kusaidia katika shughuli zake kwenye majanga ya kibinadamu.

Sauti
1'42"