Tufanye kazi kwa pamoja kutimiza haki kwa watu wenye ulemavu-Guterres
Zaidi ya watu bilioni moja duniani wana aina fulani ya ulemavu na katika jamii nyingi, watu hao wanatengwa, wanakabiliwa na upweke na unyanyapaa.
Zaidi ya watu bilioni moja duniani wana aina fulani ya ulemavu na katika jamii nyingi, watu hao wanatengwa, wanakabiliwa na upweke na unyanyapaa.
Shirika la kazi duniani, ILO, linasema utumwa bado ni tatizo kubwa linalowathiri zaidi ya watu milioni 40 duniani kote, watoto wakiwa ni robo ya idadi nzima pamoja na uwepo wa itifaki ya kuzuia hali hiyo ya kulazimishwa kufanya kazi iliyofikiwa mwaka 2016.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake,UN Women, limemteua muigizaji maarufu wa filamu Danai Gurira kuwa balozi mwema ambaye atatumia jina lake na kujitolea kwake katika kushughulikia masuala ya usawa wa kijinsia na haki za wanawake ikiwa ni pamoja na kuzipa nafasi sauti za wanawake ambazo hazijasikika.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amepokea tamko la mkutano wa nchi 20 zilizoendelea kiuchumi linaloelezea nguzo nne zilizopewa mkazo katika mkutano huo ikiwa ni mustakabali wa kazi, miundombinu ya maendeleo, maendeleo ya chakula endelevu na mkakati wa kuimarisha jinsia kwa kupima matokeo kwa watu wa jinsia tofauti ya sera zilizopangwa katika ajenda ya G20.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres kupitia taarifa iliyotolewa leo jumamosi, ameeleza masikitiko yake kutokana na kifo cha aliyekuwa rais wa 41 wa Marekani George H.W. Bush aliyefariki dunia jana Ijumaa.
Miaka 30 tangu kuanza kwa maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani, harakati dhidi ya ugonjwa huo bado ziko njiapanda.