Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa  UN António Guterres akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano wa G20 huko Buenos Aires Argentina Novemba 29, 2018
UN News/Natalia Montagna

Mkutano wa G20 wakamilika, UN yapokea azimio.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amepokea tamko la mkutano wa nchi 20 zilizoendelea kiuchumi linaloelezea nguzo nne zilizopewa mkazo katika mkutano huo ikiwa ni mustakabali wa kazi, miundombinu ya maendeleo, maendeleo ya chakula endelevu na mkakati wa kuimarisha jinsia kwa kupima matokeo kwa watu wa jinsia tofauti ya sera zilizopangwa katika ajenda ya G20.