Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Michelle Bachelet , Kamisha Mkuu  wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa
Picha na UN/Jean-Marc Ferré

Uchunguzi dhidi ya mauaji ya Khashoggi lazima uwe huru: Bachelet

Kamishina Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu Michelle Bachelet leo amesisitiza tena kwamba mauaji ya mwandishi wa habari wa Saudi Arabia Jamal Khashoggi ni lazima yafanyiwe uchunguzi huru na wa kutoingiliwa, ili kuhakikisha tathimini ya kina na uwajibikaji kwa ukiukwaji wa haki za binadamu uliotekelezwa katika uhalifu huo wa kutisha.

Taswira ndani ya Baraza Kuu wakati wa upigaji kura wa azimio namba 2439 kuhusu Ebola nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC leo tarehe 30 Oktoba 2018
UN /Manuel Elias

Baraza la Usalama lapitisha azimio kuchagiza harakati dhidi ya Ebola DRC

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa wajumbe wa Baraza la Usalama kwa kauli moja wamepitisha azimio ambalo pamoja na kuchagiza harakati za kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC , limelaani vikali mashambulizi na mauaji  ya watoa huduma za afya ambao wanaweka rehani maisha yao kutokomeza ugonjwa huo hatari.

Sauti
3'6"