KM anajiandaa kuzuru Asia
KM Ban Ki-moon anatarajiwa kuanza ziara ya siku 12 katika bara la Asia kuanzia kesho Ijumaa ambapo pia atahudhuria Mkutano Mkuu wa Mataifa Wanachama wa Kundi la G8 utakaofanyika Ujapani.
KM Ban Ki-moon anatarajiwa kuanza ziara ya siku 12 katika bara la Asia kuanzia kesho Ijumaa ambapo pia atahudhuria Mkutano Mkuu wa Mataifa Wanachama wa Kundi la G8 utakaofanyika Ujapani.
Wapatanishi wa UM na UA kwa Darfur, yaani Jan Eliasson na Salim Ahmed Salim waliwakilisha ripoti zao mbele ya Baraza la Usalama Ijumanne, kwenye kikao cha hadhara kilichosailia hali, kijumla, katika eneo hili la Sudan magharibi.
Manfred Nowak, Mkariri Maalumu wa UM juu ya Masuala ya Mateso na Vitendo Katili vya Kuadhibu na Kudhalilisha Utu ametoa mwito kwa Serikali ya Zimbabwe na jumuiya ya kimataifa wajumuike kipamoja, kidharura, kufanya kila wawezalo kusitisha haraka fujo na vitendo vya mateso nchini humo dhidi ya raia.
Kadhalika, kundi la wataalamu maalumu wa Kamisheni ya UM juu ya Haki za Bindamau hii leo wamewasilisha ripoti ya shirika iliosisitiza kuingiwa na wahaka mkubwa na khofu juu ya hali na usalama wa watu 200,000 waliongo\'lewa mastakimu na makazi katika mji wa Harare na katika sehemu nyengine 29 nchini Zimbabwe.
Baraza la Usalama, kwenye taarifa ya raisi kwa mwezi Juni, limeyasihi makundi yote yanayohasimiana Sudan Kusini kutumia mwongozo wa \'ramani ya mapatano\' yaliofikiwa Juni 8 kwenye yale Maafikiano ya Jumla ya Amani, ili kuzima cheche za fukuto liliozusha fujo za karibuni kwenye mji wa Abyei.
Taasisi za UM zinazoshughulikia juhudi za kimataifa za kukomesha mateso na kusaidia waathiriwa wa janga hili, zimetoa taarifa muhimu yenye kusisitiza kwamba walimwengu bado watahitajia kuchangisha bidii zao kwa wingi zaidi ili kufanikiwa "kuwapatia kinga na hifadhi madhubuti kila mwanadamu mstahiki dhidi ya mateso" licha ya kuwepo ulimwenguni kwa vyombo kadha wa kadha vya sheria ya kimataifa vinavyoharamisha janga hilo.
Matokeo ya ripoti ya kura ya maoni ilioendelezwa kwemye mataifa 19 mbalimbali duniani na taasisi ijulikanayo kama WorldPublicOpinion.org yamekabidhiwa UM mapema wiki hii.
David Veness, KM Mdogo anayehusika na Masuala ya Ulinzi na Usalama wa UM amemuarifu KM kwamba ameamua kujiuzulu, kwa khiyari, kwa sababu anaamini ilivyokuwa yeye ndio mwenye dhamana ya shughuli za Idara ya Usalama, ambayo ilishindwa kudhibiti hifadhi bora ya majengo ya UM mjini Algiers na kuashiria uwezekano wa kushambuliwa, aliwajibika kuwacha madaraka baada ya shambulio maututi la kigaidi kwenye majengo ya UM Algiers mnamo Disemba 2007.
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti kuwa linaendelea kushinikiza, kwa sauti kuu, aachiwe huru yule mfanyakazi wao, Hassan Mohammed Ali, ambaye alitekwa nyara Ijumamosi iliopita kutoka nyumbani kwake katika mji wa Afgooye, kilomita 30 kutoka Mogadishu, na watu wasiojulikana. Kwa mujibu wa UNHCR mateka Ali aliweza kuzungumza kwa simu na aila yake Ijumapili usiku na alisema hali yake ni nzuri; lakini taarifa nyengine ziada yoyote kuhusu mahali alipo na utambulisho wa makundi yaliomtorosha haijulikani. ~
Ijumatatu usiku, Baraza la Usalama liliafikiana, kwa kauli moja, kushtumu kampeni ya utumiaji mabavu inayoendelezwa na wenye madaraka Zimbabwe, dhidi ya wapinzani wa kisiasa, na pia kulaani vitendo vya Serikali ambavyo inaripotiwa huwanyima wapinzani haki ya kuendeleza kampeni huru za uchaguzi. Kwenye taarifa iliotolewa baada ya majadiliano ya faragha katika Baraza la Usalama, Raisi wa mwezi Juni wa Baraza, Balozi Zalmay Khalilzad wa Marekani alisema wajumbe wa Baraza wanaamini fujo iliotanda sasa hivi Zimbabwe, ikichanganyika na vikwazo dhidi ya vyama vya upinzani, ni hali ambayo uchaguzi ulio huru na wa haki hauwezekani kufanyika abadan, uchaguzi ambao umetayarishwa ufanyike Juni 27 (2008).