Baraza la Usalama lakutana tena kusailia mgogoro wa Ghaza
Baraza la Usalama limekutana Ijumatano magharibi, kwenye kikao cha dharura, kuzingatia mswada wa azimio liliodhaminiwa na Libya, kwa niaba ya Mataifa Wanachama wa Umoja wa Nchi Huru za KiArabu, kuhusu uwezekano wa kusimamisha mapigano yaliozuka katika eneo la WaFalastina liliokaliwa la Tarafa ya Ghaza. Kwenye risala mbele ya kikao hicho, KM Ban Ki-moon alikumbusha ya kuwa mtiririko wa mgogoro uliofumka Ghaza siku ya leo umeingia siku ya tano. Alisema raia wa KiFalastina, wanaojumuisha mfumo wa jamii hakika ya Tarafa ya Ghaza, pamoja na mpango wa amani kwa siku za