Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

Kwenye majadiliano ya hadhara ya Baraza la Usalama kuzingatia hatua za kuwapatia raia wanaojikuta kwenye mazinigira ya mapigano hifadhi bora, KM Ban Ki-moon alihimza kwa Baraza kuhakikisha raia wote wanaohitajia misaada ya kihali hupatiwa misaada hiyo kidharura bila ya kuchelewa.

Na kwa habari za hapa na pale

Mkurugenzi mkuu wa idara ya chakula duniani WFP Bi Josette Sheeran, ameonya kwamba wakazi maskini wa mashambani barani Afrika wanakabiliwa na kimbunga kikubwa cha nyongeza za bei za chakula, mabadiliko ya hali ya hewa na muengezeko wa idadi ya watu.