Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UM kupunguza wahudumia misaada ya kiutu katika Chad

UM umetangaza kwamba kutokana na hali ya usalama inayoendelea kuharibika katika eneo la Chad ya mashariki zile huduma za kupeleka misaada ya kihali kwa wahamiaji wa Sudan 110,000 waliopo huko zitabidi zipunguzwe pamoja na kupunguza wafanyakazi wa UM wanaohusika na kadhia hizo.

Mshoni wa Zambia kutunikwa zawadi ya UM kwa kupiga vita UKIMWI

Jonsen Habachimba, mshoni kutoka Zambia pamoja na shirika linalojulikana kama Jumuiya ya Maendeleo ya Vijiji ya Mboole (Mboole Rural Development) wametunukiwa zawadi ya dola 20,000, ikiwa ni tunzo la awali la UM kwa mashirika ya kiraia yanayojitolea kushiriki kwenye juhudi muhimu za kupambana na UKIMWI.