Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNEP yazingatia hifadhi ya mikoko katika Bahari ya Pasifiki.

Shirika la UNEP limetangaza kwamba utafiti ulioendelezwa karibuni kuhusu hali ya mikoko katika Bahari ya Pasifiki umethibitisha ya kuwa kunahitajika kuchukuliwa hatua za haraka za pamoja, kimataifa, kuhifadhi uchumi wa mfumo muhimu wa ikolojia ya eneo hilo. Mabadiliko ya hali ya hewa yalionekana kukithirisha kima cha usawa wa bahari na kuhatarisha mazingira maumbile ya eneo.

Mtaalamu wa UM athibitisha uchumi maendeleo umeshindwa kuzalisha ajira.

Charles Gore, Mtaalamu aliyetayarisha Ripoti ya UM ya 2006 juu ya Maendeleo ya Mataifa Yanayoendelea (LDC) amearifu wiki hii kwamba ijapokuwa katika 2004 maendeleo ya uchumi katika nchi masikini yaliongezeka kwa kiwango cha 5.9, muongezeko huu ulishindwa kupanua fursa za ajira na pia kutofanikiwa kupunguza ufukara na hali duni, kwa ujumla, katika maeneo hayo.