Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Lilly Kiden akibeba mazao ya mbogamboga kutoka kwa shamba lake.
FAO

Asante FAO kunijengea mnepo sasa najikimu mimi na familia yangu: Lilly Kiden

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 ukijiandaa kufunga pazia hapo kesho nakupeleka Sudan Kusini jimbo la Equatorial Mashariki ambako wakulima walioathirika na mabadiliko ya tabianchi sasa wanajengewa mnepo na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na wengi wameweza kujikwamua pamoja na familia zao. Ungana na Flora Nducha akikuletea safari ya mafanikio ya mmoja wa wanuafa wa mradi huo wa FAO. 

Sauti
2'8"
Kiwanda cha uzalishaji wa nishati ya jua kata kisiwa cha Unguja nchini Tanzania.
World Bank

Benki ya Dunia yasaidia ukuzaji wa rasilimali watu na maendeleo nchini Tanzania

Tarehe 19 Desemba mwaka 2019, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio namba 74/245, ambalo liliteua tarehe 4 Desemba kuwa Siku ya Kimataifa ya Benki kwa kutambua mchango mkubwa wa benki za maendeleo za kimataifa na benki nyingine za maendeleo za kimataifa katika kuleta maendeleo endelevu na kuchangia uboreshaji wa hali za maisha za wananchi. 

Sauti
2'5"