Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Lokua Kanza, balozi wa kitaifa wa UNICEF nchini DRC kuhusu elimu ametembelea shule aliyosoma utotoni na kusihi wanafunzi kuzingatia umuhimu wa elimu
UNICEF/Josue Mulala

Mwanamuziki Lokua Kanza atoa ujumbe kwa wanafunzi nchini DRC

Lokua Kanza, mwanamuziki nguli ndani  na nje ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye pia ni balozi wa kitaifa wa elimu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo, ametumia ziara yake katika shule ya msingi aliyosoma utotoni ili kuchagiza wanafunzi wa kike na wa kiume kupatia kipaumbele suala la elimu. 

 

Sauti
2'22"
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Peter Mathuki (kulia) akihojiwa na Leah Mushi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kando mwa Mjadala Mkuu wa UNGA76
UN News/Assumpta Massoi

Hatma ya DRC kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki mikononi mwa Mawaziri wa jumuiya hiyo

Wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa nchi duniani kuimarisha ushirikiano wa kimataifa iwe kikanda au kidunia unazidi kuitikiwa ambapo Jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC inachukua hatua kupanua wigo wa uanachama wake kutoka 6 hadi 7 kwa kufanya kikao cha kujadili ombi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kujiunga na chombo hicho. 

 

Sauti
2'9"
Wakimbizi huko Minawao, kaskazini mashariki mwa Kamerun, wanapanda miti katika mkoa ambao umekatwa misitu kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa na shughuli za kibinadamu.
© UNHCR/Xavier Bourgois

Mradi wa upandaji miti wanufaisha wakimbizi nchini Cameroon

Mradi kabambe wa upandaji miti, ulioanzishwa mwaka 2018 katika kambi ya wakimbizi ya Minawao nchini Cameroon kwa ushirikiano kati ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR na shirikisho la waluteri duniani, LWF umesaidia kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kuzuia kuenea kwa jangwa katika ukanda wa Sahel. Leah Mushi ana taarifa zaidi kutoka katika video ya UNHCR.

Sauti
1'40"