Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Manusura wa mauaji ya kimbari ya Rwanda Liberée Kayumba, mwenye umri wa miaka 24, na mfanyakazi wa WFP anayesaidia wakimbizi wanaokimbilia nchi yake.
WFP/Jonathan Eng

Lishe ya WFP iliniokoa, sasa natumikia WFP kusaidia wengine- Liberee Kayumba

Wahenga walinena ukishikwa shikamana, na ndivyo anavyofanya Liberee Kayumba ambaye ni manusura wa mauaji ya kimbari ya Rwanda dhidi ya Watutsi yaliyofanyika mwaka 1994, anasema yuko hai leo hii sababu ya msaada wa chakula wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP , ambao ulimuhamasisha baadaye kujiunga na shirika hilo kusaidia wakimbizi wa Burundi kama alivyosaidiwa.

Sauti
2'12"
Uhamishwaji wa wahamiaji wa nchi ya tatu ambao walikuwa wamekwama katika kituo cha mapokezi Misrata, Libya. (Maktaba)
IOM

Mazingira ya Libya yalikuwa tete ndio maana nikarejea nyumbani: Mhamiaji Mohamed

Kutana na muhamiaji Mohamed Ahmed Bushara aliyekwenda kusaka maisha Libya miaka mitano iliyopita lakini hali ngumu, ubaguzi , machafuko na kuwekwa rumande vilimkatisha tamaa ya kukimbiza ndoto hiyo na akakata shauri kurejea nyumbani Sudan kushika ustaaranu mwingine kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM na Muungano wa Ulaya. 

Sauti
2'22"