Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Kamanda wa kikosi cha Tanzania huko DRC, Luteni Kanali John Ndunguru (katikati) katika mazungumzo na afisa wa jeshi la DRC, FARDC huko Beni, DRC.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Saa 24 za mlinda amani TANZBATT 7 nchini DRC 

Kila mara tumekuwa tukimulika shughuli za jumla za walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu katika maeneo mbali mbali duniani iwe ni ujenzi wa barabara, ulinzi wa amani na hata kilimo lakini leo tunaangazia je mlinda amani mmoja mmoja siku yake inakuwa vipi? Na leo tunammulika Luteni Kanali John Ndunguru, Kamanda wa kikundi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT 7, kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO. Anayetuletea ripoti hiyo ni Issa Mwakalambo, Afisa Habari wa TANZBATT 7. 

 

Sauti
2'8"
Watoto wa Cambodia wakipata mlo. Watoto kukosa lishe bora husababisha unyafuzi
World Bank/Masaru Goto

COVID-19 yaongeza shida ya watoto wenye utapiamlo- UNICEF 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema kuwa nyongeza ya watoto milioni 6.7 wenye umri wa chini ya miaka mitano wanaweza kupata tatizo la kuwa na uzito mdogo zaidi kulingana na urefu wao na hivyo kuwa na unyafuzi kutokana na madhara ya kiuchumi na kijamii yatokanayo na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19

Sauti
2'37"
Watu wakifanya manunuzi katika soko la Sederek nchini Azerbaijan.
UN News/Elizabeth Scaffidi

WHO yasaidia kurejesha kwa madaktari wa Azerbaijan ili wasaidie mapambano dhidi ya COVID-19 nchini mwao 

Ikiwa ni sehemu ya msaada wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kwa harakati za Azerbaijan kupambana na virusi vya corona au COVID-19, mradi wa REACT-C19 umewaleta madaktari 19 raia wa Azerbaijan waliokuwa wanafanya kazi Uturuki ili warudi nyumbani kusaidia kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa sekta ya afya kuhusu jinsi ya kushughulikia COVID-19.

Sauti
2'22"