Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mradi wa maji warejesha matumaini kwa familia Wajir

Mradi wa maji warejesha matumaini kwa familia Wajir

Pakua

Maji ni uhai, ni kauli mbiu ya miaka nenda rudi, lakini imesalia ndoto kwa wengi duniani hasa wakati huu mabadiliko ya tabianchi yanachochea ukame unaovuruga maisha ya binadamu, wanyama na mimea. Nchini Kenya katika kaunti ya Wajir, iliyoko kaskazini-mashariki mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, uhaba wa maji ulisababisha familia kupoteza mifugo yao, mazao kukauka na ustawi wa jamii kutoweka. Lakini shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, kwa kushirikiana na serikali ya Kaunti walianzisha mradi wa ujenzi wa kuchimba visima wa Giriftu kwa ili jamii iwe na uhakika wa kupata maji wakati wowote. Mradi umezaa matunda na ndio msingi wa makala yetu ya leo inayoletwa na Assumpta Massoi.

Audio Credit
Flora Nducha/Assumpta Massoi
Audio Duration
4'24"
Photo Credit
UNICEF VIDEO